top of page
Apungua kilo 55 baada ya matibabu ya puto
“Zoezi la utoaji puto kwa Bw. Fortunatus limefanyika leo Februari 12, 2024 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kutokana na muda wa kukaa na puto kuisha ambapo linaweza kudumu kwa muda wa miezi 6 hadi 12” amefafanua Dkt. Muhondezi.
Baada ya kupoteza kilo 55 kwa mwaka mmoja, Bw. Vicent Fortunatus wa Dar es salaam aondolewa puto tumboni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila mwezi Februari 2024.
Bw. Fortunatus amefurahia matokeo ya puto na kusema kuwa afya yake imeimarika. Amesema kuwa sukari na presha yake ziko sawa, hana maumivu ya mgongo tena, mwili wake ni mwepesi na anaweza kufanya kazi zake kwa urahisi.
bottom of page